Posts

Showing posts from April 29, 2016

NDOA ZA JINSIA MOJA

Image
Huko nchini Colombia, Mahakama imehalalisha rasmi ndoa za wapenzi wa jinsia moja. Colombia inakuwa nchi ya nne kuhalalisha ndoa hizo katika mataifa ya Kilatino. @EATV

UTATA WA KIFO CHA PAPA WEMBA..

Image
Hembu angalia hii video hapa chini Mtandao wa Kinshasa-makomba.com ametoa shutuma kuwa mwimbaji Papa Wemba aliyefariki wiki iliyopita kwa kuangaka jukwani ghafla hakufariki kwa kifo cha kawaida bali amewekewa sumu kwenye mic aliyekuwa akiimbia..Mtandao huo umekwenda mbali zaidi na kuweka video ikionyesha tukio zima jinsi alivyobadilishiwa mic na kuwekewa yenye sumu....

Mwili wa Papa Wemba Wawasili Kinshasa Congo

Image
Mwanamuziki huyo ambaye ametajwa kuwa mmoja ya waanzilishi wa muziki wa kizazi kipya cha Soukous anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumanne baada ya mwili huo kuwekwa katika uwanja wa mpira kwa raia kutoa heshima zao za mwisho. Maafisa wa serikali na wanadiplomasia watahudhuria ibada ya kumkumbuka mwanamuziki huyo katika uwanja wa ndege kabla ya mwili huo kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti. Tamasha la bure la usiku kucha lilifanyika mjini Abidjan ambapo mwanamuziki huyo alianguka alipokuwa akiimba.Mwanahabari wa BBC Tamasin Ford anasema kuwa mashabiki wengi walivalia nguo nyeusi na kubeba mishumaa ili kutoa heshima kwa nguli huyo wa muziki. Mkewe Papa Wemba na wasaidizi wake pia walikuwepo.