Posts

Showing posts from May 9, 2016

AFYA; ..FAIDA YA JUICE YA MATUNDA MWILINI

Image
Juisi ni kinywaji bora na maarufu duniani, lakini ni vyeme ukajua juisi ipi ina faida mwilini na ipi haina faida yoyote. Katika zama tulizonazo, kumezuka aina nyingi za vinywaji vinavyoitwa juisi, wakati si juisi bali ni vinywaji vyenye ladha ya matunda mbalimbali. Juisi ni kinywaji kilichotengenezwa kutokana na tunda halisi au mboga na si mchanganyiko wa maji na kemikali nyingine zenye ladha ya matunda na kupewa majina kama juisi ya machungwa, nanasi, zabibu, n.k. Mara nyingi vinywaji hivyo huwekewa sukari na kemikali nyingine za kuhifahdia (preservertives) ili zisiharibike, ambavyo kiafya havikubaliki. Licha ya kutumia jusi halisi kama kinywaji tu, juisi pia hutoa kinga na tiba kwa maradhi mbalimbali. Iwapo mtu atatengeneza mchanganyiko maalum wa matunda na kutayarisha juisi maalum na kuinywa, anaweza kupata kinga na tiba ya matatizo mbalimbali ya kiafya kama ilivyoanishwa hapa chini: KAROTI+ KITUNGUU SWAUMU + EPO Juisi ya mchanganyiko wa karoti, kitunguu swaumu

AFYA: SABABU YA FANGASI UKENI

Image
Fangasi ya ukeni husababishwa na fangasi aina ya  Candida albicans . Ugonjwa huu huitwa  vaginal candidiasis  kwa kiingereza na ni kati ya magonjwa ambayo husumbua wanawake mara kwa mara. Njia za Maambukizi Fangasi ya ukeni huambukizwa kwa njia ya; Vyoo vichafu Kuchangia nguo za ndani na taulo Uwezekano wa kupata fangasi ya uke au fangasi ya uke kujirudia rudia unaongezeka pale ambapo mwanamke ana; Kisukari Ujauzito Anatumia antibiotics kwa muda mrefu UKIMWI Joto, unyevu mwingi na nguo za kubana huchangia pia kutokea kwa fangasi ukeni. Ugonjwa huu haumbukizwi kwa njia ya ngono. Dalili Fangasi ya ukeni inaweza kuleta dalili zifuatazo kwa wagonjwa wenye maambukizi; Kuwashwa sehemu za siri hasa wenye uke na mashavu ya uke. Kutokwa na maji maji meupe mfano wa maziwa kutoka kwenye uke ambayo hayana harufu mbaya. Maumivu wakati wa kukojoa kwa baadhi ya wagonjwa. Mara chache hali hii hutokea, ikisabaishwa nakuchubuka wakati wa kujiwasha. Matibabu Matibabu

MICHEZO: KESSY AJIUNGA YANGA

Image
                    Hassan Ramadhani Kessy (katikati) akitia dole gumba kwenye fomu za mkataba wa kujiunga na Yanga Kuna msemo wa Kiswahili unasema ‘ukisusa wenzio wala’, msemo huu umetimia baada ya beki wa kulia wa kikosi cha Simba SC Hassan Kessy kutia dolegumba kwenye fomu za usajili za Yanga na kujiunga na mabingwa hao wa mitaa ya Twiga na Jangwani. Kessy ametia saini juzi mkata wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka miwili kuanzia mwezi ujao (June, 2016). Awali Kessy alikuwa akiitumikia klabu ya Simba kabla ya kufungiwa mechi tano na wekundu hao wa Msimbazi kwa madai ya kuigharimu timu kutokana na kitendo cha kuoneshwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Toto Africans mchezo uliomalizika kwa Simba kupoteza kwa bao 1-0. Licha ya Simba kumfungia Kessy, tayari beki huyo mwenye uwezo mkubwa wa kukaba ns kupandisha mashambulizi mkata wake wa na Simba unamalizika mwisho wa msimu huu na klabu hiyo haikuonesha nia ya kuhitaji huduma ya nyota huyo wa z