Posts

Showing posts from August 1, 2017

JINSI YA KUFANYA USAFI WA CHUMBA CHA KULALA

Image
Chumba chako lazima ukihifadhi vizuri kwa sababu ndio mahali ambapo unapatumia wakati ukiwa umechoka na unahitaji upumzike. Ni sehem ambapo unahitaji kuondoa mawazo zote na kutuliza mwili na akili, pia ni mahali ambapo kwa wewe uliyekwenye ndoa unapata faragha ya kutosha kuwa na mweza wako. kutokana na kuwepo kwa chumba cha kulala basi ni vizuri kikawa na mwonekano utakaokufanya vizuri ukiwa ndani ya chumba chako maana ndio sehemu ya kukuondolea uchovu na mawaz sio vizuri chumba kionekane kikiwa kimejaa uchafu kama makaratasi au vitabu kila mahali bila mpangilio mzuri. pangilia vitu vyako vizuri ilikuleta mvuto ndani ya chumba chakio cha kulala,sio chumba kinakuwa kama store ya kuhifadhia mazao yakiisha vundwa Chumba kinaongezeka mvuto pale unapokipamba kwa maua, fremu za picha, mapazia mazuri na pia kapeti zuri la kuvutia. kwa wale nye familia unaweza weka picha ukiwa na familia yako au mkeo/mumeo ukutani au mezani  Nguo ziwe zimepangwa vizuri kabatini au sandukuni na