Posts

Showing posts from September 2, 2016

Satelaiti ya Facebook ya kufikisha mtandao kasi Afrika yaharibiwa

Image
 Mwanzilishi wa kampuni ya Facebook Mark Zuckerberg amelezea kusikitishwa kwake baada ya satelaiti ambayo Facebook ingeitumia kwa mawasiliano ya kasi ya mtandao wa intaneti barani Afrika kuharibiwa. Satelaiti hiyo iliharibiwa katika mlipuko uliotokea eneo la Cape Canaveral jimbo la Florida, Marekani siku ya Alhamisi. Satelaiti hiyo kwa jina Amos-Six ilikuwa imebebwa na roketi ya Falcon Nine ambayo ililipuka ilipokuwa ikifanyiwa majaribio ya kujiandaa kwa safari ya siku ya Jumamosi. Mlipuko huo ulitokea wakati roketi hiyo ilikuwa ikijazwa mafuta na kutikiza majengo yaliyokuwa umbali wa kilomita kadha. Bw Zuckerberg, ambaye yumo ziarani Afrika, amesema "nimesikitishwa sana" kusikia kwamba satelaiti hiyo iliharibiwa. "Tutaendelea kujitolea katika lengo lengo la kufikisha huduma ya mtandao kwa kila mtu na tutatia bidii hadi kila mtu apate nafasi na manufaa ambayo yangetokana na satelaiti hii," aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Mwanzilishi wa kampuni ya facebook Mark Zuckerberg amezuru nchini Kenya

Image
Mwanzilishi wa kampuni ya facebook Mark Zuckerberg amezuru nchini Kenya katika ziara yake ya mataifa ya bara Afrika. Zuckerberg aliyewasili siku ya Jumatano kutoka nchini Nigeria alifanya kikao na waziri wa habari nchini Kenya Joseph Mucheru,ambapo walizungumza kuhusu mtandao na mipango ya serikali kuhakikisha kila kijiji kimeunganishwa na mtandao. Baadaye Zuckerbag aliekea katika hoteli ya Mama Oliech katika chakula cha mchana ambapo kwa mara ya kwanza alikula Ugali na Samaki. ''Swala muhimu ninapozuru taifa lolote jipya ni kujaribu kula chakula chao.Nilipenda sana ugali na samaki mzima wa tilapia'',alisema Zuckerberg.