AFYA; Umuhimu wa mazoezi


 
Mwili wa binadamu waweza kufananishwa na nyumba inayojengwa, nyumba hujengwa kwa matofali, simenti, chokaa na malighafi nyingine nyingi, na inahitaji ukarabati wa mara kwa mara ili iendelee kuwa nyumba bora, nyumba iliyoachwa kukaliwa na binadamu huchakaa haraka na pengine hubomoka kabla ya wakati wake. Mwili wa binadamu nao kama ilivyo nyumba una mahitaji yake, unahitaji chakula bora ili uendelee kubaki katika hali ya afya nzuri,
pia unahitaji mazoezi ya viungo ili uweze kuwa imara na wenye nguvu. Mwili wa binadamu hata viumbe wengine(wanyama) unapokosa mazoezi hunyong’onyea na mifumo ya mwili hushindwa kufanya kazi vizuri inavyotakiwa.
Mazoezi ya mara kwa mara au kufanya kazi zinazohusisha matumizi ya nguvu ya mwili yanasaidia mifumo mingi ya mwili kufanya kazi inavyotakiwa, mazoezi yatatuepusha na magonjwa ya moyo, kisukari, na hata magonjwa mengine hayataweza kushambulia miili yetu, na ni njia nzuri ya kupunguza uzito wa mwili uliozidi. Unapokuwa unafanya mazoezi mara mara utafaidika na mambo yafuatayo:
Moja ni kuongeza nafasi ya kuboresha umri wa kuishi na kuishi katika afya njema.
Pili mazoezi yanasaidia kutulinda na magonjwa ya moyo, kiharusi na magonjwa yanayoambatana nayo kama shinikizo la damu na ongezeko au kiwango cha juu cha lehemu katika damu. Kiwango cha juu cha lehemu katika damu kimekuwa kisababishi cha ongezeko la shinikizo la damu na hata kuwa katika hatari ya kupata kiharusi.
Tatu mazoezi yanatusaidia kuepukana na magonjwa ya kansa fulani kama kansa ya tumbo, kansa ya matiti, kansa ya mapafu na kansa ya kizazi. Hii ni kwa sababu mazoezi yanaboresha mifumo mbali mbali ya mwili na kuwezesha mwili kutoa taka na sumu mbali mbali mwilini, pamoja na kuimarika kwa kinga ya asili ya mwili.
     Tafiti za wanasayansi zilizofanyika hivi karibuni zinaonyesha kuwa mazoezi yanasaidia kutokupoteza uwezo wa kuona. Matatizo mengi ya kuona hujitokeza mara nyingi kwa wazee, kwa hiyo tunaweza kuzuia hali hiyo isijitokeze kwa kufanya mazoezi.(kwa mujibu wa jarida la newscientist la marekani)
Pia mazoezi yanasaidia kutukinga na kisukari aina ya pili (ugonjwa ambao mtu anaupata ameshakuwa mkubwa na sio kwa kuzaliwa), na kutukinga na matatizo ya mmeng’enyo ambayo yanaweza kutuletea magonjwa ya moyo na kisukari pia.
Mazoezi yanasaidia pia kutukinga na matatizo ya mmomonyoko wa mifupa (osteoporosis) ambayo mara nyingi hujitokeza uzeeni. Yanaimarisha afya ya akili, yanasaidia kutuepusha na magonjwa ya kupoteza kumbukumbu hasa kwa wazee. Pia mazoezi yanatuondolea msongo wa mawazo, woga na mtu kuwa katika afya nzuri ya akili.
Mazoezi yanasaidia kuwa na mapafu yenye kufanya kazi vizuri,moyo wenye afya na kuimarisha misuli ya mwili kwa ujumla. Bila kusahau kuwa mazoezi husaidia kupata usingizi mzuri kwa afya bora.
Kwa hiyo basi kama mazoezi ya mara kwa mara na kazi zinazohusisha matumizi ya nguvu za mwili zina faida katika afya ya miili yetu, maisha ya ulegevu yatakuwa na matokeo ambayo ni kinyume chake.

Popular posts from this blog

SIFA ZA MWANAMKE MNENE KITANDANI NA RAHA YAKE.

mazoezi kwa ajili ya kufanya uke uwe tight(mnato)

Faida ya kula BAMIA -na kazi yake mwilini

KAZI YA SHANGA KIUNONI NA MAANA YA RANGI ZAKE........