MAHITAJI SITA YA KIHISIA KWA MWANAUME

1. Kuaminika (Trust) - Mwanaume anahitaji kuaminika. Ni vizuri sana kujua unaaminiwa. Kuhusiana na maamuzi ya kifedha, Maamuzi yanahusiana na malezi, n.k. Kwa mwanaume kuhisi anaaminiwa, Mwanamke anahitajika kuwa mu-wazi na kueleza mahitaji yake pasipo kificho ama hila. Kwa kuwa hili ni jambo la asili kwa mwanamke, mwanamme anatakiwa kuwa makini kwa mwanamke anapokuwa anazungumza. Anapofanya hivyo, hitaji la kwanza la msingi la kihisia la mwanaume linakuwa limetimizwa. Endapo mwanamme anahisi kuwa anaaminiwa, hitaji la mwanamke la kujaliwa nalo linakuwa limetimizwa.
2. Kukubalika (Acceptance) - Wakati unapoweza kwa dhati na kwa uwazi kumpokea mwanaume na "mapungufu yake" yote, anahisi kukubalika. Hili ni la muhimu kwa afya ya hisia za mwanaume katika mahusiano. Mara ya kwanza, unaweza usihisi kama anafanya kile unachotaka afanye ili kukusaidia. Kama utamkubali kwa jinsi alivyo na ukafanya juhudi za kupata msaada zaidi pale ambapo unakuwa unauhitaji, atajihisi kukubalika. Mwanaume anapojihisi kukubalika kwa jinsi alivyo, inakuwa ni rahisi kwake kutimiza mahitaji ya msingi ya mwanamke ya kumwelewa.
3. Kutambulika (Recognition) - Umewahi kusikia msemo "Watoto huililia, Wanaume huifia". Tunaongelea Kutambulika. Hakuna kilicho kizuri kama kutambulika kwa kufanya kazi nzuri, hata katika mahusiano yako. Kutambulika ama kuthaminiwa kwa juhudi zako, hata katika mahusiano yako. Kutambulika ama kutahaminiwa  kwa juhudi zako kwaweza kwenda mbali. Wakati ambapo wanaume wameweza kutambuliwa mchango wao wanajua kuwa mchango wao si bure ama kuwa inachukuliwa kirahisi na watakuwa tayari kuridhisha hisia za tatu za wake zao zinazohusu kuheshimiwa (Respect)
4. Shauku (Admiration) – Kuwa na shauku na mumeo kwa urahisi ni kumuweka katika viwango vya juu vya kujali na kumfurahia. Mwanamume anapohisi kuwa anaheshimika kiwango hicho, nguvu zake hujitokeza kwa kung'aa. Kwamba ni mchekeshaji, Mwenye nguvu, Mkweli, anavutia kimapenzi (romantic), n.k. Sifa zote hizi zinajitokeza kwa uwazi zaidi pale mke anapoonesha kuwa na shauku ya mumewe. Mwanaume anapoona shauku hii toka kwa mkewe, Hitaji la nne la mke la uaminifu (Loyalty) linakuwa limetimizwa.
5. Kuthibitika (Approval) – Hili ni kubwa lakini pia dogo. Kuthibitika ni jambo dogo kiasi kwamba kama halikueleweka, laweza kufanya madhara zaidi kuliko wema. Kwa lugha ya picha, hili ni hitaji la msingi la mwanamke la kihisia pia isipokuwa kuna tofauti ndogo. badala ya "kuthibitisha" mwanamke anahitajika kuthaminiwa (Validated). Kwamba anakubali ama anakataa. Kila mwanamme anapenda kuwa shujaa kwa mkewe. Hii haimaanishi kuwa lazima ukubaliane na kila kitu anachofanya au kusema. Kuthibitisha kwako inamaanisha kuwa unamtambua na kuheshimu kwa mambo mema anayofanya katika mahusiano yenu.
6. Kutia moyo (Encouragement) – Mwanaume anahitaji kutiwa moyo na mkewe. unapomtia moyo mkewe, inampatia tumaini na ujasiri kukupatia mahitaji yako yote ya msingi ya hisia za kimahusiano. Wakati ambapo mke anamuamini, Kumkubali, Kumtambua na kuwa na shauku na mumewe, hili linamtia hamasa ya kuendelea kutimiza mahitaji yote ya kihisia ya mwanamke.
 
@marriage family

Popular posts from this blog

SIFA ZA MWANAMKE MNENE KITANDANI NA RAHA YAKE.

mazoezi kwa ajili ya kufanya uke uwe tight(mnato)

Faida ya kula BAMIA -na kazi yake mwilini

KAZI YA SHANGA KIUNONI NA MAANA YA RANGI ZAKE........